Thursday, March 28, 2024
spot_img
HomeUncategorizedBuriani Walibora

Buriani Walibora

Kakamega

Collins Chibole na James Boaz Eshitemi

Kifo cha Prof Ken Waliaula walibora huenda ndilo pigo kubwa Zaidi kuwaikutokea kwa ulingo wa Kiswahili na waenzi wa kazi zake.Hadi kifo chake,Ken Walibora amekuwa mlezi wa wengi katika ulimwengu wa kiswahili.

Kando na waandishi, walimu na wahadhiri wengi ambao walikikumbatia Kiswahili katika maandishi, Walibora aliichangamkia lugha ya Kiswahili pia katika baghwabaghwa za kila siku hususan kama mwanahabari na pia kupitia kampeni za kuimarisha lugha ya Kiswahili.

Prof Ken Walibora

Tuzo tatu mtawalia alizopokea za Jomo Kenyatta literature prize kufuatia vitabu vyake, Ndoto ya Amerika, Kisasi Hapana na Nasikia Sauti ya Mama, zinapeana taswira ya mwandishi aliyeumiliki ulimwengu fulani katika uandishi wa lugha. Marehemu amejipatia sifa kutokana na uandishi wake uliokosha wengi, uchapishaji na uhariri vyote ambavyo alifanya kwingi ikiwa ni pamoja na Kidagaa Kimemwozea

Siku Njema, Ndoto ya Amerika,Kisasi Hapana, Nasikia Sauti ya Mama,Damu Nyeusi, Nizikeni Papa Hapa miongoni mwa nyingine.

JAMES BOAZ ESHITEMI

JAMES BOAZ ESHITEMI

Japo  kwa  wengi   yaonekana  habari ila   kwangu  itasalia  jinamizi   manake  yanikwepa  maneno  mahususi ya  kumrejelea  shujaa, jagina na  gwiji  ‘mungu’ wa  waswahili  Ken  Waliaula  almaarufu  Walibora .

Mwaka  wa  2005 nikiwa shule  ya  msingi  ya  Eshiakhulo  wilayani  Mumias  kaunti  ya  Kakamega  ndipo ilikuwa  kaski  yangu  ya  kwanza  kusikiza  habari, mawazo  na  ulumbi  wa  mwandishi  huyu  mahiri  kupitia  kwa  vitabu  alivyoandika.

Riwaya ya  Siku Njema ,Ndoto ya Almasi na  Kufa  Kuzikana  ni  miongoni  tu mwa  gange  zake  zilizonivutia  katika shule  ya msingi  kutokana  na  jinsi  alivyozichambua  mwalimu  Lina  Akacha, kabla  ya  kujiunga  na  shule  ya  upili ya Lubinu  nilikokutana  na  bwana  Odali  Victor  aliyenipa motisha  ya  kuendeleza  kukisoma  kiswahili  na  hata  kukizungumza.

Japo  kwa  mukhtasari kutokana   na  kazi  yake Ken  Walibora  nimeweza  kufunza lugha  pana ya  kiswahili,  kufanya  katika  vituo  kadha vya  utangazaji,kando  na  kuwa mhutubu   katika   makongamano  anuwai hapa  nchini kenya.

Baadaye  nilijiunga  na  chuo kikuu  cha  Masinde  Muliro kama  mwalimu  wa  lugha  ya  kiswahili tokea  mwaka  wa  2013 nilikoichangamkia  lugha  hii aula  ya  Kiswahili. Japo  kwa  athari  za  lugha  mame  mara  nyingi  tulijifunga   kibwebwe  na  kusaliti  mila  zetu  kwa  kuiasi  lugha  mame.  Kiswahili  kiliniezesha  kuisatili  jamaa yangu  kwa  kuienzi  kazi yake.  

Mazishi ya Ken Walibora

Japo  kwa  mukhtasari kutokana   na  kazi  yake Ken  Walibora  nimeweza  kufunza lugha  pana ya  kiswahili,  kufanya  katika  vituo  kadha vya  utangazaji,kando  na  kuwa mhutubu   katika   makongamano  anuwai hapa  nchini kenya. Japo  kwa  kumbukizi zake  Ken  Walibora  ni  kwamba  mti  mkuu umeanguka  ila  viziki vingali na rotuba linapochomoza shamzi kwa wengi huwafikia mwangaza ila kwa wachache huwafaidi. Kwa wengi hunyaa mvua ila kwa wachache huipata mbegu ya kutia arthini.

Amewalea  wanahabari  chipukizi  kando  na kuvipalilia vipaji chipukizi  katika  Nyanja  za  Kiswahili. Itakumbukwa  kuwa Prof  Ken  Walibora  amekuwa  kielelezo  kwa  waandishi  wenzake, wanahabari, Na hata  walimu kwa  ujumla  bila  kuwasaza waenzi  asharafu  wa  lugha  pana  ya  Kiswahili  na  tanzu  zake.

Prof  Ken  Walibora  amekuwa  nguzo muhimu katika  tasnia  nzima  ya Kiswahili  na wapenzi  wake. Ina  maana Walibora  amekuwa  ‘mungu’  wa  waswahili.

Mazishi ya Ken Walibora

Amewalea  wanahabari  chipukizi  kando  na kuvipalilia vipaji chipukizi  katika  Nyanja  za  Kiswahili. Itakumbukwa  kuwa Prof  Ken  Walibora  amekuwa  kielelezo  kwa  waandishi  wenzake, wanahabari, Na hata  walimu kwa  ujumla  bila  kuwasaza waenzi  asharafu  wa  lugha  pana  ya  Kiswahili  na  tanzu  zake.

Tangia  lugha  ya  Kiswahili  kufanywa  linkua franka nchini  kenya  Prof  Ken  Walibora  amekuwa  mstari  wa  mbele  katika  kukilonga  Kiswahili   haswa katika  miktadha   tofauti tofauti ikiwemo  makongamano,  katika  vyuo  vikuu,taasisi mbalimbali  ikiwemo  shule  za  upili  na  zile  za  msingi.

Lugha  aliyoitumia  mwandishi  Ken  Walibora  katika  kazi  zake  ilikuwa lugha  ya  kipekee  iliyosheheni  ufundi  wa  kipekee. Ken  Walibora  pia  ameichora  taswira  ya  matabaka mawili; tabaka la wakwasi na  lile  la  walalahoi.

Walibora  alitoa  mtafaruku uliopo  katika  uongozi  kando  na  kuichora  picha  kamili  inayojitokeza  wazi  kati  ya  walio  na  kisomo  bila  ajira  na wenye ajira bila kisomo katika ukinzani.  Kwa  kauli  yangu, mwandishi  Ken  Walibora   licha  ya  kututangulia  mbele  ya  haki  atasalia  katika  nyoyo  zetu  kama  waenzi  wa  lugha  ya Kiswahili kutokana na vile alivyokua na  ufundi  wa  namna  yake  katika  tasnia  nzima  ya  Kiswahili. 

Mchango  wako  utatulazimu  tukuite  hayati. Nani  anakujua  ni  msamiati  ambao   umekula  wengi  na  hata  kuwaelekeza  wengi  wa  adinasi  ahera. Siku  zote  umesema  chema  hakidumu … uru Ken Walibora safiri salama mfahamishe JALALI KUWA  CHINI WINGU NI SAMAWATI  KWA  KULITAZAMA.

COLLINS CHIBOLE

COLLINS CHIBOLE

Nakumbuka nikiwa darasa la nne, babangu aliponitunuku kitabu cha siku njema baada ya kuongoza somo la Kiswahili shule ya msingi ya Eshisenye, ikawa riwaya yangu ya kwanza kuisoma maishani na ukawa mwanzo wa ndoto yangu katika uandishi.

Namtambua Walibora kama aliyechangia pakubwa kufanikiwa kwangu katika lugha ya Kiswahili katika mitihani ya Kitaifa ya KCPE na ya KCSE. Kando na taaluma yangu ya ujasiriamali na fedha, kazi ya walibora ndiyo iliyonisukuma kuandika riwaya yangu ya kwanza ya ‘Nyota ya Mama’ kando na tamthilia ya ‘Fumbo la Imani’.

Walibora ni mwanahabari aliyeumiliki ufundi wa kutamaniwa, mkufunzi na mwandishi aliyeukumbatia ucheshi na ulumbi wa kupigiwa mfano. Si ajabu kwamba , marehemu katika uandishi wake alisisitiza kuwa kila nafsi ni sharti itayaonja mauti, kuna visa si haba vya ubashiri ambavyo vinarejelea kifo chake.

Nilipojiunga na radio MMUST FM mwaka 2013, nilianzisha Makala ya ‘Kisiwa cha Lugha’ na moja kwa moja Walibora akawa mlezi wa Makala hayo licha ya shughuli nyingi zilizomsetiri.

Walibora ni mwanahabari aliyeumiliki ufundi wa kutamaniwa, mkufunzi na mwandishi aliyeukumbatia ucheshi na ulumbi wa kupigiwa mfano. Si ajabu kwamba , marehemu katika uandishi wake alisisitiza kuwa kila nafsi ni sharti itayaonja mauti, kuna visa si haba vya ubashiri ambavyo vinarejelea kifo chake.

Kutoka kwa ufukara, kongowea mswahili mhusika mkuu katika riwaya ya siku njema mwishoni analitazama wingu la magharibi na tabasamu la ufanisi, milki ya babake ikiwa chini yake pamoja na binti  Vumilia tamanio la moyo wake.

Kwa mfano katika riwaya ya siku njema, ‘mwili wa Mzee Kazikwisha ulipatikana na mwanawe Msanifu Kombo siku kadhaa baada ya kifo chake. Hakujulikana na wengi kuwa alikuwa Juma Mukosi,msomi wa kutajika, maziko ya juma mukosi yalihudhuriwa na idadi ndogo ya watu’. Mtemi Nasaba Bora katika riwaya ya Kidagaa Kimemwozea alipatikana akiwa ameipa dunia kisogo na mazishi yake kuhudhuriwa na idadi ndogo ya watu. Uandishi wa walibora unasetiri ujumbe wa Tumaini.

Kutoka kwa ufukara, kongowea mswahili mhusika mkuu katika riwaya ya siku njema mwishoni analitazama wingu la magharibi na tabasamu la ufanisi, milki ya babake ikiwa chini yake pamoja na binti  Vumilia tamanio la moyo wake.

Mto kiberenge katika riwaya ya Kidagaa kimemwozea, licha ya kuwa ulisetiri laana na kutafsiriwa kuwa hatari kwa yeyote ambaye angeyanywa maji yake, Imani na Amani wahusika wakuu baada ya kuyanywa maji yake walitulizwa kiu na hatimae haki yao kupatikana na mmoja wao kupendekezwa hata kuwa mfalme katika jamii hiyo. Mti mkuu ushavunjika ila kupitia kazi zake, atazaa, atalea, atakuza, ataelimisha na kuhamasisha. Rabi ailaze roho yake mahala pema.

Mwisho.

RELATED ARTICLES

1 COMMENT

  1. Very creative and good story,ken has not died but rested,naona akina ken wengine hapa ,

    #collins chibole , nakufuatilia pole pole jinzi unavyoteremusha Kiswahili yako ,utaenda mbali sana

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
Google search engine

Most Popular

Recent Comments

Rodgers Wakhisi on Buriani Walibora